Menu ›
Burudani
Thu, 27 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' ameweka wazi kuwa, ataachia Ngoma Mpya wikiendi hii.
Akiwa Instagram Live, Diamond amesema kwamba atatoa Ngoma Mpya akiwa Mjini Berlin huko nchini Ujerumani ambapo ataenda kufanya show siku ya Jumamosi Aprili 29, 2023.
Diamond Platnumz anatarajia kutumbuiza katika Tamasha La AfroFest 2023 na wasanii wengine kutoka Nigeria kama Young Jonn. Tamasha Hili limeandaliwa Na Balafon_eu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live