Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Diamond ayakumbuka mahaba ya Wema Sepetu

5006 Diamond And Wema Chibu Perfume Diamond ayakumbuka mahaba ya Wema Sepetu

Sun, 5 Sep 2021 Chanzo: eatv.tv

Staa wa muziki nchini Tanzania Diamond Platnumz amefunguka kwamba kila akiitazama video ya wimbo mpya ya naanzaje anakumbuka mahaba mazito ya Madam akimaanisha Wema Sepetu.

Diamond ameshea hilo akipromote video yake hiyo kwenye mtandao wa Instagram kisha akaandika maneno yafuatayo

"Nikiitazama hii video, hususan kipande hiki nakumbuka mbali sana...enzi za mahaba mazito na Madam, enzi ambazo tulikuwa tunajifungia chumbani wiki nzima, nakwepa ku-record na hata show ikitokea naitaftia sababu ya kutokuwepo"

"Kiukweli wimbo huu wakati nautoa sikuuchukulia serious, niliutoa tu kama 'bonus' kwa kujua mashabiki zangu wameni-miss kunisikia nikiimba hivyo licha ya kupokelewa na kupendwa sana ulivyotoka"

"For some reason kadri muda uendanvyo nimejikuta naupenda sana mbaya zaidi kila niusikiapo unanifanya nitamani tena kumpenda mtu na kuwa tena wenye mahusiano japo ghafla akili timamu hunijiagna kunambia Simba jifocusie zako kwenye kazi mwaya"

Couple ya Diamond Platnumz na Wema Sepetu ni moja kati ya couple iliyokuwa gumzo nchini Tanzania ambayo ilianza mwaka 2010 na kuachana 2014.

Chanzo: eatv.tv