Menu ›
Burudani
Tue, 21 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa muziki wa Bongo Fleva Diamondplatnumz ameeleza kuwa maisha hayaitaji chuku ili mtu afanikiwe.
Diamond ameeleza hayo kupitia ujumbe alioandika kwenye uwanja wa komenti katika video fupi iliyowaonesha wachekeshaji Tx Dullah na Ndaro wakicheza wimbo wake mpya wa komasava aliouachia wiki mbili zilizopita. Ameandika,
"Natamani sana vijana wengi waelewe ya kuwa kwenye maisha haiitaji kumpandikizia mtu chuki ili wewe ndio ufanikiwe, inatakiwa tu ubunifu, juhudi, nidhamu na kumuomba mwenyezi Mungu naye atakufungulia kila kitu kitawezekana tu."Ameandika Diamond.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live