Mkurugenzi wa Wasafi Classic Baby na msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ameingia kwenye trend ya aina yake baada ya kutoa pua!
Video fupi iliyosambaa mtandaoni imemuonesha Diamond akiwa nchini Malawi kwenye wataalamu wa masauala ya hereni ambapo mhusika alichukua mashine maalum ya kutobo pua na kuweka heleni kwenye tobo hilo.
Kitendo hicho kimemelea maoni mengi hasi kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengi walimkumbusha wimbo wake wa Muziki Gani alioimba na Nay wa Mitego.
Kwenye wimbo huo, kuna mstari Diamond alisema; “kazi yenu kutoboa pua..” mstari huo alikuwa akimchana Nay wa Mitego kwamba wasanii wa Hip Hop wanatoa pua.