Msanii wa Bongofleva toka WCB Wasafi, Diamond Platnumz ameshangaa kupungua uzito ghafla hadi kufikia Kg 73.9!.
Hatua hiyo inakuja miezi miwili baada ya msanii huyo kulazwa hospitali hapo Desemba 25, 2022.
Hivi karibuni baadhi ya mashabiki mtandaoni kudai msanii huyo kapungua mwili. Doh! 73.9kg,” aliandika chini ya video inayomuonyesha akiwa amesimama juu ya kifaa cha kupima uzito wa mwili na kuambatanisha ujumbe huo wake na emoji zinazoashiria mshangao mkubwa.
Hata hivyo, hii sio mara ya kwanza kwa Diamond kupungua uzito, iliwahi kutokea hadi Meneja wake na WCB Wasafi kwa ujumla, Babu Tale akazungumzia hilo.