Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' amenusurika kifo baada ya kukwama kwenye lifti akiwa na kruu lake.
Diamond ameshea kipande cha video ambacho wamejirekodi akiwa na mabaunsa wake ndani pamoja na wapambe wake wakiomba msaada kwa fundi baada ya kuhangaika kwa muda mrefu.
Kwa jitihada za fundi wa lift hiyo ambayo hawajaitaja ni ya jengo gani, mwishoni alifanikiwa na kuwatoa wakiwa hoi. Diamond aliandika ujumbe huu kwenye ukurasa wake wa Instagram:
"Siku ya leo mimi @juma_jux @fole_x na wenzetu kadhaa tumenusurika kifo kwenye Lifti....Ndugu zangu wenye majengo marefu yenye kutumia lifti tujitahidi kuzifanyia serivices hizi lifti zetu ili kuepusha madhara kwa Wananchi.