Kwa Mujibu wa Mtandao wa Africa facts zone umeripoti kuwa Msanii Diamond Platnumz 'Simba' anamiliki nyumba 11 nchini Tanzania, nyumba 4 Kenya, nyumba 2 Afrika Kusini.
Diamond anamiliki pia Hoteli, TV station pamoja na Radio Station pia msanii huyo anamiliki kisiwa chenye thamani ya zaidi ya Tsh bilioni 1.8 kilichopo Visiwani Zanzibar.
Pia Afrika Face Zone wameripoti kuwa Diamond huwa analipwa zaidi ya Tsh milioni 236 kwa shoo moja, huku akiingiza zaidi ya Tsh milioni 70 kwa mwezi kupitia endorsements.
Mondi anasemekana kuwa analipwa mkwanja wa zaidi ya Tsh milioni 80 kila mwezi kwenye mtandao wa YouTube.