Msanii wa Tanzania, Revokatus Kipando, almaarufu Baba Levo,amejitokea hadharani na kusimulia furaha yake huku akionesha gari la kifahari ambalo alisema kuwa lilinunuliwa na msanii Diamond Platnumzs kwa ajili ya mtoto wake.
"Nina furaha sana hata baada ya msanii Diamond kulaghaiwa Tsh Billioni 4 ana huwezo wa kununulia mtoto wangu gari la kifahari ya zaidi ya milioni mbili na nusu, gari hilo amelinunua kwa ajili ya mtoto wangu kutembelea anapopelekwa kliniki," alisema.
Msanii huyo ambaye kwa mara nyingi kwenye mahojiano humtaja Diamond kama babake wakati wa mahojiano hayo alitoa kauli akisema kuwa Diamond alimnunulia mtoto wake gari kwa kuwa ni babu yake.
"Mtoto wangu amenunuliwa gari ili na babu yake Diamond Platnumzs hili wakati anaposafiri awe kwa gari nzuri," alisema Baba levo.
Haya yanajiri siku chache baada ya Msanii almaarufu Baba Levo, kuwashagaza wengi baada ya kufunguka wazi akisema kwamba anamchukulia Diamond kama Babake mzazi na anataka awekwe kwenye urithi wa mali yake.
Kwenye mahojiana msanii huyu aliongeza kuwa yeyote anayekerwa na jambo hilo aelekee mahakamani kumshtaki kwani Diamond ndio mzazi anayemsaidia kwa maisha yake.