Kupitia Insta Story yake, supastaa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amepost kipande cha video kinachotafsiriwa kama ni kumkana mwanaye Dylan aliyezaa na mwanamitindo Hamisa Mobeto.
Kitendo hicho ambacho Diamond ameonekana akisema Dylan si mtoto wake kimetafsiriwa kama fedheha kwa mtoto huyo mdogo ambaye hajui lolote kuhusu tofauti za wqzazi wake.
Kutokana na kitendo hicho wadau mbalimbali wamemtaka Diamond na ndugu zake Wote, na kumuomba radhi mtoto huyo kwa sababu.
Hivi karibuni kuliibuka stori za kwamba Dylan si mtoto wa Diamond badala yake ni mtoto wa msanii mwenzake, Billnass jambo lililoibua hisia na mitazamo tofauti miongoni mwa mashabiki na hata Mobeto mwenyewe na familia yake ambao ni wazazi wa mtoto huyo.