Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' ameendelea kuigusa jamii baada ya leo kumuhakikishia mrembo Jackline (aliyepata ulemavu kwenye ajali) kuwa atahakikisha anapata kolabo na Staa wa Bongo Fleva, Zuhura Othuman 'Zuchu' ili kukuza kipaji chake na jina.
Jackline ambaye amefika kwenye kipindi cha Mashamsham kuomba msaada kwa Watanzania amepata dili hilo baada ya kusema kuwa mbali na kutaka msaada wa matibabu pamoja na elimu, pia ana kipaji cha kuimba ambacho angependa kukiendeleza.
Ahadi ya Diamond Platnumz imeelezwa na Steve Nyerere wakati wa mahojiano maalum kwenye kipindi cha Mashamsham.