Menu ›
Burudani
Thu, 23 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz kupitia kwenye Instastory (Instagram) yake amezionesha tuzo zake Tatu alizoshinda kutoka #MagicVibeAward ambapo kwenye ugawaji wa Tuzo hizo zilifanyika kwenye ukumbi wa #MlimanCity iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Kupitia kwenye Tuzo hizo ambazo Diamond ameshinda ni; King of The East African 2023, Vibe Entrepreneurship 2023, pamoja na Best East African Live Act 2023.
Tuzo hizi za Diamond zinakuja ikiwa ni siku chache baada ya hasimu wake, harmonize kushinda tuzo tatu za AEAUSA kwa mpigo nchini Marekani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live