MSANII Naseeb Abdul, Diamond Platnumz anayetamba na EP yake ya FOA amesema anaheshimu Tuzo za Muziki zinazotarajiwa kutolewa nchini April 1, 2022 na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) hata hivyo ameomba ashiriki tuzo za kimataifa zaidi.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Basata, Matiko Mniko amesema amepokea ujumbe wa kiongozi huyo wa WCB ambaye yeye pamoja na wasanii chini ya lebo yake hawajajitokeza kushiriki tuzo za Tanzania Music Awards 2022 (TMA) ambazo zinaratibiwa na Basata.
Basata imetangaza orodha ya wasanii wanaowania vipengele mbalimbali katika tuzo hizo ambazo zaidi ya wasanii 1360 waliomba kushiriki.