Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Diamond ajiachia na Zuchu Sauzi

Diamond Zuchuuuu Diamond ajiachia na Zuchu Sauzi

Sun, 26 Nov 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz alimsurprise Zuchu kwa dinner ya kimahaba kwa siku yake ya kuzaliwa.

Bosi huyo wa WCB anaweza kuwa mmoja wa watu walio na shughuli nyingi zaidi kwenye sekta ya burudani, lakini alichukua muda na akaenda umbali mrefu hadi kwa mwanamke maalum katika maisha yake, na kuhakikisha kuwa mchezaji wa Jazz anawakaribisha wawili hao wakati wanapanda ngazi kwa surprise kubwa zaidi.

Zuchu alifikisha miaka 30 siku chache zilizopita. Alivaa gauni la rangi ya kijivu na nywele zake zilizotengenezwa vizuri. Diamond alivalia vazi jeusi lililojumuisha suruali na shati kwa wakati huo.

Mandhari yalionyesha kiwango chao cha kisasa. Zuchu ambaye alionekana kuvutia kweli aliongozwa na Diamond ambaye alimshika kiuno huku akimhimiza atembee na kuona ni kiasi gani amemfanyia.

Timu iliyowafuata ilinasa tukio hilo huku wawili hao wakifurahia surprise hiyo nzuri.

Hata akampa shada la maua, na yeye akaringa nalo, "Ohh, Asante, hii ni nzuri asante habibi," alimwambia kuhusu matukio ya kimapenzi.

Diamond alitoa chupa ya shampeni wakiwa wamekaa kwa ajili ya chakula cha jioni. Zuchu kisha aliinamia kwa busu kutoka kwa mtu wake, huku akivua miwani yake ya jua.

Tukio alilochagua la muziki lilionyesha tabia ya kimapenzi ya Diamond. Zuchu alitoa machozi huku Diamond akimtazama akijifuta machozi. Alishikilia glasi yake ya mvinyo akimngoja ajitengenezee kabla hawajakunywa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live