Menu ›
Burudani
Fri, 8 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
SUPASTAA wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz leo Ijumaa, Oktoba 8, 2021 anatajia kutupa karata yake ya kwanza Mjini Atlanta kwenye tour yake ya kimuziki nchini Marekani.
Kwa mujibu wa ratiba yake #Diamond anatarajia kufanya shoo 11 nchini humo katika miji mbalimbali. Tour hiyo inayoanza leo, itafikia tamati Oktoba 31, 2021.
Aidha, Diamond amerejea Marekani ikiwa ni miezi kadhaa tangu akanyange ardhi hiyo, alipohudhuruia hafla ya utoaji wa tuzo za BET 2021 ambapo alikuwa anawania tuzo ya Best International Act.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live