Menu ›
Burudani
Wed, 17 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Supastaa wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amesema kuwa alianza kupambana na muziki miaka 10 kabla ya kutoka.
Diamond amesema hayo usiku wa kuamkia leo kwenye Mkesha wa Mwenge wa Uhuru Viwanja vya Sakura Pangani Tanga.
"Mimi nilianza ku-hustle na kupambania ndoto ya kuwa Mwanamuziki tangu mwaka 1999 lakini nilitoboa mwaka 2009, ni takribani miaka 10, hivyo nawashauri vijana wenzangu msikate tamaa ya kupambania ndoto zenu," amesema Diamond.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live