Menu ›
Burudani
Thu, 27 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Big boss wa Wasafi Classic Baby (WCB), Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amefunguka kuwa yeye ni shabiki mkubwa wa msanii wa lebo hiyo Mbosso.
Diamond amefunguka kuwa, alianza kuwa shabiki wa Mbosso kabla hata hajaanza kufanya naye kazi lakini imetokea wamefanya naye kazi, kwake ni heshima kubwa na anajivunia.
“Mbosso namkubali sana ndio maana unaona mbali na kufanya naye kazi napenda kuwa naye kwa sababu ni msanii ambaye namkubali,” alisema Diamond.
Mbosso anatarajia kudondosha albamu yake fupi (EP) Alhamisi hii Oktoba 27 maeneo ya Bahari Beach jijini Dar.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live