Dar es Salaam. Wasanii wa Tanzania, Diamond Platnumz, Harmonize na Ali Kiba watakutana katika tuzo za Afrimma zitakazotolewa Oktoba 27, 2019 nchini Marekani.
Mtandao wa Afrimma unaonyesha kuwa Diamond na Ali Kiba wanachuana katika vipengele viwili vya msanii bora wa kiume Afrika Mashariki na mburudishaji bora.
Katika tuzo hizo Diamond atatoa burudani jukwaani sambamba na Ommy Dimpoz na Nandy. Wasanii 13 wa Tanzania wanawania tuzo katika vipengele mbalimbali.
Harmonize, Jux, Ommy Dimpoz na Rayvanny wameingia katika kipengele cha wasanii bora wa kiume Afrika Mashariki.
Vanessa na Nandy wameingia kwenye kipengele cha wasanii bora wa kike Afrika Mashariki.
Pia yupo Kenny ambaye ni mwongozaji wa video za muziki, watayarishaji wa muziki Kimambo na S2Kizzy; Bujini na Rabbit Cre 255 ambao ni wacheza shoo, DJ Ommy katika kipengele cha maDJ na mtangazaji wa redio Times, Lil Ommy.
Pia Soma
- Samia azungumzia uharibifu wa mazingira nchi za Sadc
- Watu 16 wameuawa katika maandamano Ethiopia
- Rais Morales ashinda muhula mwingine Bolivia