Mwimbaji maarufu wa Nigeria Davido Adeleke anasema amekusanya zaidi ya Tsh. Milioni 630 kwa siku moja kutoka kwa marafiki zake pamoja na mashabiki.
Mwimbaji huyo aliwaomba marafiki zake wamtumie naira milioni moja kila mmoja kabla ya siku yake ya kuzaliwa.
— Davido (@davido) November 18, 2021
Katika ujumbe wa video uliotumwa na mwimbaji huyo alisema alitaka marafiki zake kila mmoja ampe naira milioni 100, na kwa siku moja Davido alichapisha kwenye akaunti yake ya Twitter kuwa amekusanya zaidi ya naira milioni 114 wakati yeye alikua na kiasi cha Naira milioni 83 kwenye akaunti yake kabla ya kuanza kupokea miamala.
Miongoni mwa marafiki wa mwimbaji huyo ambao walisema walimtumia pesa hizo ni E-money, Obi Cubana, Tiwa Savage Femi Otedola, Naira Marley na wengine.