Menu ›
Burudani
Wed, 22 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamuziki Davido amepewa siku yake maalumu na Meya wa mji wa Atlanta nchini Marekani #AndreDickens baada ya kutambua mchango wake katika mji huo.
Uamuzi huo umefanywa na Bodi ya Makamishna wa Baraza la Jimbo la Fulton likiongozwa na Meya Andre baada ya kuona mchango wa Davido katika kuupa heshima na kuuthamini mji huo kupitia kazi zake za muziki.
Kufuatia nyaraka hizo zilizosainiwa na Meya huyo zinaeleza kuwa kila ifikapo Novemba 21 itakuwa ni ‘siku ya kumthamini Davido’ ndani ya jimbo la Fulton na kila ifikapo Novemba 18 itakuwa siku ya Davido Atlanta.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live