Menu ›
Burudani
Wed, 17 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwimbaji star wa Nigeria Davido ameweka salio la akaunti yake ya benki katika kurasa yake ya Twitter na kusema kuwa mashabiki wake wamenitumia fedha nyingi ndani ya saa moja mara baada ya kuwaomba wafanye hivyo.
— Davido (@davido) November 17, 2021
— Davido (@davido) November 17, 2021
"Kama unaujua kuwa kuna nyimbo niliimba na ikakupendeza .. nitumie pesa," Davido aliandika katika ukurasa wake wa tweeter kabla hajaanza kushirikisha kiasi ambacho wametumiwa.
Baadae aliandika kuwa amepata naira milioni 7 sawa na dola $16,000 ndani ya dakika 10, na kutania kuwa alikuwa amelenga kupata naira milioni 100 kwa sababu alikuwa anataka kulipia deni la gari alilochukua kwa mkopo aina ya Rolls-Royce.
Ujumbe wake wa mwisho kwa twitter unaonesha amepata naira milioni 97.
Davido ana wafuazi milioni 9.7 katika mtandao wa Twitter.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live