Mwimbaji wa Nigeria ‘Davido’,amempongeza msanii mwenzake ‘Rema’ kwa kufanikiwa kupenya kwenye anga ya muziki wa Amerika.
Remix ya ‘Rema’, “Calm Down” aliyomshirikisha Mrembo ‘Selena Gomez’ hivi karibuni imeweka rekodi ya kihistoria kuwa wimbo wa kwanza Barani Afrika na Nigeria kukaa mwaka mzima kwenye chati za Billboard ya Marekani.
Katika mahojiano ya hivi karibuni kwenye kipindi cha “The Kris Fade Show”,mkali wa Afrobeats ‘Davido’ amedai hakuwahi kufikiria kuwa msanii yeyote wa Nigeria angeingia kwenye chati.
Hata hivyo,ameshangazwa na jinsi ‘Rema’ kuendelea kusalia kwenye 5 Bora kwa wimbo wake katika kipindi cha miezi 8 iliyopita.
“Miaka iliyopita,Sikuwahi kufikiria kuwa msanii wa Nigeria angekuwa na rekodi 5 bora Amerika,Rema amefanya hivyo kwa miezi 8 iliyopita,bila kutikiswa,Yeye ni msanii bora,Nakumbuka nilikuwa Dubai miaka iliyopita na nikaona baadhi ya watu wakikoshwa na nyimbo zangu,Nilifurahi sana kuona hivyo,” amefunguka ‘Davido’.