Menu ›
Burudani
Tue, 15 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamuziki kutoka Nigeria, Davido amefunguka kuwa 'albamu' yake mpya aliyoiachia mwanzoni mwa mwaka huu ya Timeless imebadilisha maisha yake.
Hii inakuja baada ya kuulizwa swali kuhusiana na 'albamu' ipi ndio imembadilishia maisha yake na kumuingizia mkwanja mwingi, Davido kupitia ukurasa wake wa Twiter, ame-share 'kava' ya 'albamu' hiyo akilijibu swali hilo aliloulizwa mtandaoni.
Albamu hiyo yenye nyimbo 17 ilitoka Machi 31, 2023, na kuvunja 'rekodi' kwa kusikilizwa mara nyingi siku ya kwanza tu baada ya kuachiwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live