Menu ›
Burudani
Mon, 29 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Dkt Kedmon Mapana leo amekutana na Msanii kutoka katika lebo ya muziki nchini WCB Wasafi, D-Voice kwa lengo la majadiliano yenye kujenga tasnia ya Muziki.
Aidha, katika majadiliano hayo Katibu Mtendaji alimpitisha katika kitabu cha Mwongozo wa Maadili katika kazi za Sanaa.
Majadiliano haya yamefanyika leo 29 Januari 2024 katika ofisi za Katibu Mtendaji BASATA zilizopo Maeneo ya Kivukoni jijini Dar es salaam.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live