Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Coolio: Rapa wa wimbo wa Gangsta's Paradise afariki dunia

Rapa Afariki Coolio: Rapa wa wimbo wa Gangsta's Paradise afariki dunia

Thu, 29 Sep 2022 Chanzo: bbc

Rapa wa Marekani Coolio, anayefahamika kwa wimbo wa Gangsta's Paradise, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 59.

Meneja wake wa muda mrefu Jarez Posey aliviambia vyombo vya habari vya Marekani kuwa msanii huyo alipatikana akiwa hajitambui kwenye sakafu ya bafuni katika nyumba ya rafiki yake huko Los Angeles.

Coolio alianza kufanya muziki miaka ya 1980, lakini aliimarisha nafasi yake katika historia ya hip hop alipotoa wimbo wa Gangsta's Paradise mnamo 1995.

Sababu kamili ya kifo chake siku ya Jumatano bado haijawekwa wazi. Hata hivyo Posey aliiambia TMZ, ambayo iliripoti habari hiyo kwa mara ya kwanza, kwamba wahudumu wa afya waliamini kuwa huenda alipatwa na mshtuko wa moyo.

Coolio, ambaye jina lake halisi lilikuwa Artis Leon Ivey Jr, alishinda Grammy kupitia wimbo wake wa Gangsta's Paradise, ambao ilitumika katika filamu ya Dangerous Minds iliyochezwa na Michelle Pfeiffer.

Wimbo huo mbaya unaendelea kusikilizwa na watu wengi na umesikiliwa na zaidi ya watu bilioni moja kwenye Spotify, kwa mujibu wa tovuti hiyo.

Zaidi ya kazi yake iliyochukua miongo minne alirekodi Albamu nane na kushinda Tuzo ya Muziki za American Music Award na Tuzo tatu za Muziki za Video za MTV.

Vibao vyake vingine ni pamoja na Fantastic Voyage, Rollin' With My Homies, 1, 2, 3, 4 (Sumpin' New), na Too Hot.

Chanzo: bbc