Menu ›
Burudani
Wed, 10 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii nguli wa Bongo Fleva, Chid Benz amewashangaza Baadhi ya Mashabiki zake pamoja na wasanii baada ya kuonekana akiwa Kanisani kwa Nabii Geordavie.
Katika video iliyosambaa mitandaoni, Chid ameonekana akifika kwenye madhabahu ya kanisa la mchungaji huyo huku akichechemea na kumweleza kuwa ameungua na moto kwenye mguu.
Baada ya maelezo hayo, Nabii Geordavie alionekana kufurahia ujio wa Chid Benz ambapo alimuombea na kumpatia kiasi cha fedha kwa ajili ya kujikimu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live