Mwanamuziki Rashid Makwiro maarufu Chid Benz amesema kuwa amewahi kumpenda mwanadada mmoja ambaye hata hivyo alikuja kuambulia maumivu baada ya kutendwa vibaya.
Chid amesema hayo wakati akihojiwa na chombo kimoja cha habari nchini kuhusu maisha yake binafsi na maisha ya muziki wake.
"Kuna mwanamke niliwahi kumpenda ana akili sana lakini alikuja kunifanyia tendo ambalo nilikuja kuamini kwamba hakuna mwanamke yoyote mwenye akili.
Unajua kwanini nasema hamna akili? Nilimpenda, nilimwamini, nilikuwa na mkumbatia nilikuwa nafanya vitu ambavyo sijafundishwa kufanya, nafanya nilivyoona kwenye movie, naongeza ambavyo sijui nafanya nini lakini nilikuwa najua ana akili, najua ananipenda then nikimtumia meseji hajibu anajibu baadae hivyo tuishie hapo Love is crazy," amesema Chid Benz.