Baada ya Chesco kukiri kwamba moyo wake umekuwa haujiwezi kimahaba kwa Love Juakali na kuamua kumtongoza na kuishia kufokewa kwa maneno makali na mwanadada huyo bila kukata tamaa, Love amemjibu.
Love amesema Chesco sio type yake wala aina ya wanaume anaovutiwa nao kimahusiano hivyo haitokuja kukaa wakawa wapenzi.
Love ameweka wazi kwamba ni wazi Cheaco anatafuta kiki kupitia jina lake hivyo aandike ameula wa chuya. Love amesema ni kweli yeye ni mweusi ila hawezi kuwa na mwanaume mweusi kama yeye.
Pamoja na hayo Love amekuwa moja ya waigizaji walioteka hadhira kupitia tamthilia maarufu ya Juakali pia amekuwa akivutia watu kwa kujiamini kwake kwa kiwango cha juu.