Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chege sasa avunja ukimya

718a495917773b39145110a6aae50eb7 Chege sasa avunja ukimya

Sun, 29 Nov 2020 Chanzo: habarileo.co.tz

MSANII mkongwe nchini Saidi Hassani 'Chege Chigunda' anatarajia kuachia wimbo wake mpya baada ya ukimya wa muda mrefu.

Kupitia kwenye ukrasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram ameshapisha vipande vya wimbo huo ambao ameshirikisha mwanadada Rose Ree.

Chege aliyewahi kuvuma na Kundi la TMK Wanaume lilokuwa linamilikiwa na Said Fella picha zinaonesha yupo studio na Rose Ree wakiimba pamoja.

Chege siku za hivi karibuni aliwahi kunukuliwa na vyombo vya habari nchini kuhusiana na kazi yake alidai ukimya wake ulikuwa na maana kubwa kusoma mazingira ya tasnia hiyo .

"Unajua kazi hizi tunazofanya zinahitaji kuwa mbunifu kila wakati, sio vibaya kukaa kimyaa kwa muda kuangalia na kusoma wenzako wanakuja kwa mtazamo upi Ili kulikamata soko, " alisema.

Chanzo: habarileo.co.tz