Menu ›
Burudani
Mon, 31 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
MSANII mkongwe wa muziki kutoka nchini Uganda, Joseph Mayanjais maarufu kama Jose Chameleon ameushangaza umma baada ya kutaka siku akifariki basi azikwe na jeneza la kioo kwa kuwa katika msiba wake watahudhuria watu wengi kutoka mataifa mbalimbali.
Katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha luninga cha NBS nchini Uganda, Chameleon amesema kuwa haogopi kufa kwa namna yoyote ile kwani msiba wake utatengeneza pesa nyingi sana.
Amesema Chameleon; “Nataka niwe na sanduku la kioo ili kila mtu anione kwa sababu watu wengi watahudhuria mazishi yangu kutoka nchi kadhaa."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live