Menu ›
Burudani
Thu, 29 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamuziki kutoka Marekani Catherine Janice Ipsan, maarufu kama Cat Janice (31) amefariki siku ya jana kwa ugonjwa wa kansa.
Taarifa za kifo cha Cat Janice zimetolewa kwenye ukurasa wake wa Instagram ambao kwa sasa unasimamiwa na Kaka yake.
Mwezi wa kwanza mwaka huu Cat Janice alijizolea umaarufu duniani baada ya kutoa wimbo wake "Dance You Outta My Head.", Wimbo huu ulifanya vizuri TikTok pia kwenye chart za Billboard.
Cat Janice ameacha mume "Kyle Higginbotham" na mtoto mmoja wa kiume mwenye umri wa miaka 7 "Loren".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live