Mwanamitindo maarufu nchini, Calisah Abdul, amejigamba kuwa ni miongoni mwa watu wenye DM nyingi zaidi za wanawake Afrika Mashariki ambazo hajajibu.
Calisah ametoa kauli hiyo baada ya mrembo kutoka Kenya Shakila kudai kuwa anataka kulipwa Dola 50 ili kujibu DM za watu huku Calisah alikuwa na DM zake kibao.
Calisah ameandika; “Hawa Ndo Maslay Quen wanaosema wanataka walipwe kujibu DM Anyways, nina mastaa wenu zaidi ya 23 in my DM na bado sina time.
"I don’t think kuna mtu ana DM nyingi za wanawake zaidi yangu East Africa, I have been that guy my whole life.”
Calisa pia amesema kuanzia sasa atatoza Tsh 350,000 kujibu DM za warembo.