Menu ›
Burudani
Fri, 13 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwimbaji wa Nigeria Burna Boy ametajwa tena kutumbuiza kwenye tamasha kubwa la Muziki nchini Marekani #Coachella mwaka 2023.
Burna Boy ametajwa kwenye orodha ya wasanii ambao watatumbuiza siku ya Ijumaa April 14 pamoja na wakali Bad Bunny, Pusha T, Becky G, Metro Boomin na wengine.
Tamasha hilo ambalo huenda kwa wikendi mbili, mwaka huu litaongozwa wakali kama Calvin Harris, Frank Ocean, Blackpink na Bad Bunny. Hii inakuwa mara ya pili kwa Burna Boy kutumbuiza kwenye Jukwaa kuu la tamasha hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live