Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Burna Boy aweka rekodi Boomplay

Burna Boy E1555408815415 Burna Boy aweka rekodi Boomplay

Tue, 5 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwimbaji wa Nigeria aliyeshinda tuzo ya Grammy, Damini Ebunoluwa Ogulu, almaarufu Burna Boy, amekuwa msanii wa kwanza kukusanya streams bilioni moja kwenye jukwaa la muziki wa kidijitali, Boomplay.

burna alipata mafanikio hayo kufuatia kutolewa kwa albamu yake ya saba ya studio, “I Told Them.”

Ukitazama kwenye akaunti yake ya Boomplay inaonyesha kwamba mwimbaji huyo amekusanya zaidi ya streams bilioni moja kwenye jukwaa hilo.

Boomplay ni jukwaa kubwa zaidi la streaming za muziki wa kidijitali barani Afrika. Ilizinduliwa mnamo 2015. Burna Boy pia ndiye msanii anayefuatiliwa zaidi kwenye jukwaa na wafuasi zaidi ya 600,000.

Mwimbaji huyo wa “African Giant” ndiye msanii wa kwanza wa Nigeria kuvuka utiririshaji wa kazi bilioni 1 kwenye Apple Music, Spotify, YouTube, Audiomack na Boomplay.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live