Msanii maarufu wa muziki nchini Nigeria, Burna Boy ameonekana kwenye private party ya supastaa wa muziki Duniani, Beyonce iliyofanyika Paris nchini Ufaransa.
Katika picha ambayo imesambaa tangu jana ikimuonyesha Burnaboy akimkumbatia Beyoncé ambapo ni watu wachache pekee wamealikwa kwenye party hiyo.
Hii sio mara ya kwanza Burna Boy Kuwa karibu na Beyonce. Itakumbukws kwamba Album ya Soundtracks zinazopatikana kwenye Filamu ya The Lion King (2019), Album hii ilifanywa na Beyonce na Miongoni mwa wasanii ambao wameshirikishwa kwenye Album hii ni Burnaboy.
Mbali na Burnaboy, mwanamama Beyoncé aliwapa shavu Wasanii kadhaa kutoka Afrika, Wizkid (Brown skin Girl), Mr Eazi, Yemi, Shatta Wale, Busiswa, Tiwa Savage, Tekno.
Mashabiki wengi wa Burnaboy baada ya kuona picha hii akiwa na Beyoncé wametamani wawili hawa kufanya kolabo.