Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Buda Alazimika Kufichulia Mke Kuhusu Mpango wa Kando Tapeli

0fgjhs18i1fruqe6tg Buda Alazimika Kufichulia Mke Kuhusu Mpango wa Kando Tapeli

Thu, 25 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mzee mmoja tajiri mwenye afisi jijini Nairobi alilazimika kufichua siri zake za michepuko kwa mkewe ili kujinusuru kutoka kwa mpango wake wa kando aliyekuwa akimtapeli.

Hii ni baada ya mrembo huyo ambaye alikuwa amechumbiana na mzee kwa miaka saba kutishia kuanika siri zao mbele ya mkewe baada ya penzi lao kuingia doa.

Kulingana na Taifa Leo, matatizo yaliibuka baada ya kipusa kumtaka mzee kumtumia KSh 20,000 kila siku, jambo ambao lilimshtua sana buda ambaye alianza kumfokea.

“Je, umesahau ulivyojisifu tulipokutana kwa mara ya kwanza? Kwamba wewe hupokea zaidi ya elfu hamsini kila siku? Iweje ulielie kwamba nakufilisi. Tuma pesa la sivyo, najua alipo mkeo. Naweza kuenda wakati wowote naikamweleza jinsi tumekuwa tukimla kivuli miaka hiyo,” demu alitishia.

Inasemekana buda aliingia baridi kwa siku kadhaa akiwa hajui namna ya kufanya kujinasua katika mtego wa kidosho na ikambidi kila siku atafute elfu ishirini amtumie kipusa.

“Naona zimeingia, jikaze mzee,” mrembo alikuwa akimwelezea buda kila alipopata arafa ya hela.

Hata hivyo, buda alishindwa na kasi ya mwendo ambayo dada alikuwa akimpeleka na akaamua kumwangukia miguuni mkewe kufichua yaliyokuwa yakiendelea katika maisha yake.

“Mke wangu najua nilikukosea na naomba radhi. Kuteleza si kuanguka. Naomba msamaha wako,” jamaa alilia huku akimwelezea mkewe kila kitu.

“Shukran kwa kunieleza. Nilikuwa nimesikia fununu na nikajinyamazia. Mradi hutachepuka tena nimekusamehe,” mke alimwambia mumewe.

Duru zinaarifu kuwa kisima cha pesa kilipoanza kukauka, demu alipandwa na hasira na kufululiza hadi kazini kwa mkewe.

“Je, una habari mumeo alikuwa mpenzi wangu kwa muda mrefu?” kidosho alisema akijua angelipua mambo.

“Hilo nalifahamu na tayari nimemsamehe. Ondoka hapa kabla sijawaita polisi, tapeli wewe,” mke aliwaka.

Inasemekana mrembo alibaki mdomo wazi. Kwa aibu kubwa alishika njia akaenda zake akijua mambo yamemwendea mrama.

Tangu siku hiyo alikoma kabisa kumpigia mzee simu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke