Menu ›
Burudani
Thu, 1 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Meta, Mark Zuckerberg ameomba radhi kwa familia zinazodai watoto wao waliathiriwa na maudhui ya mitandao ya kijamii.
Zuckerberg ambaye anamiliki WhatsApp Instagram na Facebook amesema hayo katika mkutano wa Bunge nchini Marekani ambapo ulihusisha viongozi wa Tiktok, Snapchat, X(Twitter) na Discord.
Hata hivyo Wabunge walitaka kujua hatua zinazochukuliwa kuwalinda watoto mitandaoni, ambapo pia walizungumza na baadhi ya familia ambazo zilisema watoto wao walijidhuru na wengine kujiua kutokana na maudhui ya mitandao ya kijamii.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live