Bodi la Filamu la Kenya (KFCB) imeipiga marufuku filamu ya Rafiki ambayo ndani yake inagusia mapenzi ya jinsia moja.
Bodi hiyo imepiga marufuku filamu hiyo kuonyeshwa hadharani au kutangazwa kwenye televisheni na kusambazwa, ikisema maudhui ya filamu hiyo inayoonesha mapenzi ya jinsia moja kati ya wanawake wawili, inakiuka sheria za Kenya.
Muongozaji na muandishi wa filamu ya Rafiki, Wanuri Kahiu, kupitia mtandao wa Twitter amethibitisha kufungiwa kwa filamu hiyo.
“I am incredibly sorry to announce that our film RAFIKI has been banned in Kenya. We believe adult Kenyans are mature and discerning enough to watch local content but their right has been denied. #Cannes2018 #AKenyanFirst,” ameandika Wanuri.