Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Black Panther yazidi kutikisa dunia, yaingiza dola bilioni 1.182

5017 Black Panther Poster TZW

Tue, 20 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Filamu ya ‘Black Panther’ imezidi kufanya vizuri katika mauzo yake duniani.



Filamu hiyo imetajwa kuingiza kiasi cha dola milioni 605.4 kwa Marekani ndani ya mwezi mmoja tangu ilipotoka February 16 ya mwaka huu, pia imeingiza kiasi cha dola bilioni 1.182.5 duniani kote.

Kutokana na kiasi hicho kilichoingiza filamu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya Marvel Studios, imevunja rekodi zilizowahi kuwekwa na filamu kibao kwenye box office.

Black Panther ambayo imeongozwa na Ryan Coogler, ilitumia bajeti ya kiasi cha dola milioni 200–210 katika kuitengeneza.

Black Panther imewakutanisha waigizaji kama Chadwick Boseman ambaye ndio staa wa filamu hiyo, Lupita Nyong’o, Michael B. Jordan, Danai Gurira, John Kani na Connie Chiume.

Chanzo: bongo5.com