Menu ›
Burudani
Fri, 3 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Hip Hop Bongo, Billnass amesema mipango yake kwa siku za mbeleni ni kuja kusaini wasanii wapya katika rekodi lebo yake, Mafioso Inc ambayo imekuwepo tangu mwaka 2021 ikisimamia kazi zake.
Kufanikisha hilo Billnass ataungana na mkewe Nandy ambaye kupitia lebo yake, The African Princess ameshamtambulisha msanii mmoja, Yammi aliyetoa EP moja, Three Hearts (2023) yenye nyimbo tatu.
Utakumbuka Billnass alitoka rasmi kimuziki chini lebo ya Rada Entertainment baada ya kuachia wimbo wake, Raha (2014) ambao aliwashirikisha TID na Naziz kutokea nchini Kenya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live