Staa wa Hip Hop, Billnass amezungumzia ishu ya yeye kuambiwa ni msanii atakayekuja kuziba pengo la marehemu Rapa Godzillah.
Akizungumza na Clouds FM, Billnass mume halali wa msanii wa Bongo Fleva, Faustina Chales Mfinanga 'Nandy' amesema Kibongobongo hakuna watu wa kusaka vipaji na kwamba yeye alitoka kivyake.
"Mimi nilikuwa nafanya muziki wangu hata sijui nitatoka lini. Walionisaidia ni MwanaFA na TID, awali kabisa Mchafu ambaye ndiye alianza kunisaidia ambaye nipo naye mpaka leo, hizi mambo huwa wanasema mashabiki lakini kimsingi zinakuwa kwetu zinakuwa haziakisi ukweli," alisema Billnass.