Msanii Bien Sol amezua gumzo mitandaoni baada ya kukataa kutegemewa kuupeleka muziki wa Kenya kimataifa, wakenya wamemchagua yeye kuupeleka muziki kimataifa ila kwa upande wake amegoma akisema yeye anaimba kwa ajili yake na aliletwa kwenye hii dunia kuimba, hivyo wasimtegemee kubeba msalaba wa mtu.
Msanii Bien Sol amezua gumzo mitandaoni baada ya kukataa kutegemewa kuupeleka muziki wa Kenya kimataifa, wakenya wamemchagua yeye kuupeleka muziki kimataifa ila kwa upande wake amegoma akisema yeye anaimba kwa ajili yake na aliletwa kwenye hii dunia kuimba, hivyo wasimtegemee kubeba msalaba wa mtu. Aliongeza kwa kusema ataimba hadi siku atakapotoweka duniani, ni vyema kwa sasa kila mtu apige kazi na likija swala la yeye aende ama asiende international hiyo ni shida yao wakenya wenyewe.