Menu ›
Burudani
Fri, 17 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Inadaiwa kuwa James Dolan ambaye ni mfanyabiashara na mmiliki wa ukumbi maarufu nchini Marekani wa Sphere ulioko Las Vegas, yupo kwenye mazungumzo na mwanamuziki Beyonce kwa lengo la kutaka msanii huyo afanye show katika ukumbi huo ili uweze kutambulika zaidi.
Hata hivyo inadaiwa kuwa timu ya #Beyonce imetaka kiasi cha dola milioni 10 ambazo ni zaidi ya tsh bilioni 20 kufanikisha msanii huyo kukubali kufanya show ndani ya ukumbi huo.
Beyonce alimaliza ziara yake ya "Renaissance World Tour" mwezi uliopita ambapo hajatangaza show wala ziara yoyote kwa mwakani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live