Mwanamuziki Beyonce atabiriwa kuingiza zaidi ya Shilingi Bilioni 490 za Kitanzania kupitia ziara yake ya RenaissanceWorldTour anayotarajia kuianza Wikiendi hii nchini Sweden.
Kwa mujibu wa Forbes wameandika kuwa kutokana na gharama za Tiketi na wingi wa watu wataoingia kwenye ziara hiyo ni wazi kutaenda kumfanya Beyonce kuwa msanii aliyeingiza pesa nyingi zaidi kupitia ziara za muziki na kumfanya kuvuna kiasi hiko cha pesa.
Kiingilio cha chini kwenye ziara hiyo ni Dola za Kimarekani $700 ambazo ni sawa na zaidi ya Shilingi Milioni 1.5 za Kitanzania. Beyonce anatarajia kumaliza ziara yake September, 2023.