Baada ya Staa wa Muziki wa R&B @iambenpol siku ya jana kulalamika kuwekwa kwenye orodha ya Mastaa watakaokuwepo kwenye uzinduzi wa album ya @juma_jux, mambo yalibadilika baada ya Ben kumkataa msanii huyo.
Ben Pol alifunguka na kusema kuwa hajaalikwa na wala hakuna makubaliano yoyote, kati ya management ya wasanii hao kuhusu kuhudhuria uzinduzi wa albam hiyo ya #KingOfHearts.
Imefahamika kuwa, hatimaye mastaa hao wameyamaliza na kuelewana, hivyo sasa Ben Pol atakuwepo siku ya leo kwenye uzinduzi huo.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram wa #BenPol ameandika; "Barabara zote kuelekea #TheSuperDome #Masaki leo. It’s @juma_jux #KingofHearts Day! Asante kwa kikao chetu cha leo #MoreLoveLessEgo ❤️ We gon turn up TONIGHT! #PartyModeOn."