Hatimaye King wa RnB, Ben Pol amerejea na project yake ya nyimbo 4 ambayo ameiita ‘’B’’ inayoelezea mambo mbalimbali kuhusu mapenzi huku ikiwa amemshirikisha Rapper Billnass pekee kwenye "Kisebusebu".
Submitted by Telesphory on Ijumaa , 30th Jul , 2021 Picha ya Msanii Ben Pol
Kwenye project hii Ben Pol ameimba chungu na tamu za mapenzi, kuvunjika moyo, kuwa mraibu kutokana na mahusiano na majuto kwa kutopewa nafasi ya pili ya kurekebisha makosa kwa mpenzi wake.
B imeundwa na nyimbo kama "For you, Unaita, Warira na Kisebusebu" ambazo zimetayarishwa na Chatta Vintage, Jaco Beatz na O Righty