Menu ›
Burudani
Mon, 9 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Leo Agosti 9,2021. Msanii Beka Flavour amefunguka stori za kuibiwa mpenzi wake Happy Reuter na msanii wa filamu Patrick Kanumba kwa kusema stori hiyo haijamuumiza na ameona ni vitu vya kawaida.
"Hizo nimezichukulia poa tu hazijawahi kuniumiza, nimeona ni vitu vya kawaida sana hivyo vitu vipo na kila siku vinatokea, kuhusu story za baby mama wangu tuziache kwa sasa" amesema Beka Flavour
Kwenye mahusiano yao Beka Flavor na mama mtoto wake Happy wamebahatika kupata mtoto mmoja wa kiume aitwaye Aaryan Beka flavour.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live