Menu ›
Burudani
Tue, 3 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii kutoka Nigeria, Bayanni ameeleza jinsi alivyoanza kuwasiliana na msanii Gigy Money na kwamba ni washkaji.
Bayanni amefunguka hayo jana alipokuwa akifanya mahojiano na Clouds FM akiwa nchini.
"Nilianza naye urafiki mtandaoni, tukaendelea hivyo. Tulitaka kufanya ngoma lakini kuna mambo yalitokea ikashindikana lakini naamini ipo siku tutafanya," alisema Bayanni.
Bayanni alimalizia kwa kusema Gigy si mpenzi wake bali ni marafiki na yeye yupo single.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live