Baunsa wa msanii Kizz Daniel kutoka nchini Nigeria, Kelvin Atobiloye almaarufu kama Kelvin Power ameingia katika vitabu vya kumbukumbu.
Hii ni baada yakuwa baunsa huyo kuajiri baunsa mwenzake kama mlinzi kwake binafsi kutokana na umaarufu wake alioupata gafla baada ya kupostiwa na Kizz Daniel katika mitandao yake.
Kizz alimpost Power baada ya kufanya `Challenge' ya wimbo mpya wa Kizz (My G), jambo lililomfanya mlinzi huyo kufahamika katika kila pembe ya Dunia kutokana na ukubwa wa jina la bosi wake.
Hata hivyo inasemekana pia Kizz Daniel alimuongezea mshahara baunsa wake takribani Naira millioni 2 (sawa na Tsh milioni 6.36) akisema kwamba ameufanya wimbo wake kuwa maarufu mno.