Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Barnaba aifungia kazi albamu yake

10117 35156175 780779412312313 5463476826061930496 N TZW

Thu, 28 Jun 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa Bongo Flava, Barnaba ameweka wazi kuwa amekamilisha albamu yake ambayo inatarajiwa kutoka mwezi ujao.



Albamu ya muimbaji huyo ambayo inakwenda kwa jina la Gold itakuwa na nyimbo zipatazo 18. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ndipo ameeleza kukamilika kwa albamu hiyo.

“Narudia tena kusema hii ni Gold na mgodi umebeba dhaabu ambazo zimepikwa muda mrefu sana, sitaki kusema mengi I can’t wait kwa kweli,” amesema Barnaba.

Awali albamu hiyo ilipangwa kutoka February 2018 lakini ikahairishwa hadi July 2018 kutokana na kile Barnaba alichoeleza kuwa wadhamini wake wakuu watatu walipendelea hivyo.

Mwanzoni mwa mwaka huu katika kipindi cha The Playlist, Times Fm, Barnaba alisema albamu hiyo itakutanisha wasanii wengine kutoka Kenya Uganda na Nigeria.

Wasanii waliotajwa kuwepo katika albamu hiyo ni pamoja na Juliana Kanyomozi na Jose Chameleon kutoka Uganda. Kutoka Bongo kuna Vanessa Mdee, G Nako, Ben Pol, Aslay, Barakah The Prince, Linex na Joh Makini.

Loading...
Chanzo: bongo5.com