Menu ›
Burudani
Wed, 16 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kufurahia siku kadhaa za ndoa yake, mwimbaji staa wa Bongofleva Barnaba Elias Mohamed 'Barnaba Classic' ametamba kwa kusema mke wake Raya Ally Sykes 'Raya the Boss' ndiye mzuri kuliko watu wote duniani na kama ukibisha kwenye hilo basi wewe ndio mbaya kuliko wote duniani.
Barnaba na Raya walifunga ndoa Julai 13, 2023 nyumbani kwa mama mkubwa wa Raya maeneo ya Masaki Jijini Dar es Salaam na sherehe yao ikafanyika kesho yake, Julai 14, katika ukumbi wa Mlimani City.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live